Saturday, December 15, 2012

Mike Tyson akanusha ‘uzushi’ kuwa amejigeuza mwanamke


Hatimaye bondia na bingwa wa zamani wa mchezo huo Mike Tyson amelazimika kuongea baada ya kuzuka kwa habari kuwa amefanyiwa upasuaji na kujibadilisha kuwa mwanamke.

Mitandao na magazeti mengi ya Afrika iliingizwa mkenge na habari hiyo iliyoandikwa na website ya NewsBiscuit kuwa bingwa huyo amefanyiwa upasuaji huo.

Ili kuuthubitishia ulimwengu kuwa habari hiyo ni ya uongo, Tyson ametoa maelezo kupitia mtandao wa SpyGhana na kusema:

“I am still a man and I have always been fully in touch with my masculinity and have no intention of becoming a woman.
The claims are not only untrue but unbelievably stupid. I was at the Pacquiao-Marquez fight on Saturday and any reasonable person could tell I was looking like a man.”


No comments:

Post a Comment